Breaking News

Mabweni shule ya sekondari Serengeti yateketea kwa moto.


Serengeti.Wanafunzi 200 wa wa Shule ya Sekondari ya Serengeti iliyoko kata ya Uwanja wa Ndege wilayani Serengeti Mkoa wa Mara hawana mahali pa kulala baada ya mabweni yao kuteketea kwa moto leo.

Makamu mkuu wa shule hiyo, Juvenary Chacha alisema moto huo ulianzia choo cha bweni na kusambaa taratibu na kuingia sehemu ya bweni huku jitihada za kuuzima zilizokuwa zikifanywa na wanafunzi na walimu zikishindikana na kulazimika kutoa taarifa Zimamoto na ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo.

CHANZO:MWANANCHI


No comments