Dkt. Mwakyembe asema ubadhilifu,wizi,rushwa na ufisadi wachangia Kudidimiza uchumi .
Waziri wa katiba na sheria Mh. Dkt. Harrison Mwakyembe amesema ubadhilifu,wizi,rushwa na ufisadi umechangia kwa kiasi kikubwa Kudidimiza ukuaji wa uchumi wa nchi na hivyo kusababisha hali ya umasikini kwa wanachi walio wengi huku wachache Wakineemeka na ndio maana serikali ya awamu ya tano haipo tayari kuona rushwa inapata nafasi kwa njia yoyote ile.
Mh.Mwakyembe ameyasema hayo katika uzinduzi wa wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha siku ya maadili Kitaifa na haki za binadamu ambapo amesema rushwa kwa sasa haina nafasi tena. Naye waziri wa nchi ofisi ya rais na utawala bora Mh. Angelah Kairuki amesema sheria na kupambana na rushwa inatoa adhabu Ndogo kwa wale wanaobainika na hivyo kulisasabishi hasara taifa na hivyo wanataka sheria hiyo imbane mhusika kulipa hata hasara zilizotokana na kosa lake.
Valentino Mlowola ni mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU amesema wamekuwa wakipokea taarifa nyingi za watu wakilalamikia utendaji wa ofisi za serikali na utekelezaji wa viwango vya chini wa miradi ya umma huku mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na utawala bora Mh. Tom Bahame Nyanduga akisisitiza watendaji kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi wao

No comments